What!!? U have not Subscribed yet??? Eh nga you are a RISK -TAKER!!
NOW NEW CLIPS EVERY WEEK!!!
pls also like me on facebook
https://www.facebook.com/pages/Kansiime-Anne-Entertainer/263758240421584?ref=ts&fref=ts
Kansiime Anne follows Job’s example – African comedy.
Vichekesho kati ya mume na mke kanisani
Je unajua vichekesho kanisani? ulishasikia mojawapo, hebu fuatilia hii hapa.
Kulikuwa na familia moja ya wacha Mungu vizuri tu pale Dar es salaam. Walikuwa wakisali kanisa moja la kilokole. Mwanaume alikuwa na tabia ya kulala usingizi kila akiingia ibadani. Siku moja mke wake akagundua dawa ya kumfanya jamaa aache kabisa tabia hiyo mbaya ya kulala kanisani. Unajua ni dawa gani hiyo?
Kukiwa tu ndo ibada imeanza, jamaa alianza kuuchapa usingizi na mke bila kukawia akamminya kwa haraka akamwambia,
Mke:
“Mchungaji amekuteua ufunge ibada kwa maombi”
Mwanaume akasimama haraka na kuanza kushusha maombi makali ya kufunga ibada
Mume:
“Baba katika jina la Yesu tunakushukuru kwa ibada nzuri, Asante kwa ujumbe wa leo kutoka kwa mtumishi wako Mchungaji, Asante kwa miujiza ya uponyaji. Tunaomba ututangulie tunapokwenda majumbani kwetu kupumzika, Kanisa woote tuseme Amen”
HAKUNA ALIYESEMA AMEN badala yake baada ya kumaliza sala tu, alilishuhudia kanisa nzima likimkodolea macho huku wengine wakicheka sana, na wengine wakiwa midomo wazi na wengine wakiinama kwa aibu kwani ibada ndo tu ilikuwa imeanza na jamaa anashusha sala ya kufunga ibada!
hii kali.
Nimesikia kuwa huyo bwana aliacha hiyo tabia ya kulala lakini sikujua mahusiano yake na mke wake yaliendelea kuwa mazuri au la.
Kansiime Anne wants to INVEST
What!!? U have not Subscribed yet??? Eh nga you are a RISK -TAKER!!
NOW NEW CLIPS EVERY WEEK!!!
pls also like me on facebook
https://www.facebook.com/pages/Kansiime-Anne-Entertainer/263758240421584?ref=ts&fref=ts
Vituko na Vichekesho vya Mmasai na Mpogoro
Kule Morogoro katika kibanda cha kuuzia vinywaji baridi kulitokea vichekesho vya mmasai mmoja na mpogoro mojawapo ya hivyo vichekesho hiki kidogo lakini inachekesha na kuvunja mbavu.
Kijana mmoja wa kimasai mtanashati, mwenye umri wa wastani alikwenda kujipatia kinywaji baridi katika kibanda hicho cha mpogoro.
Fuatilia mazungumzo yao:
Kijana wa kimasai alimsogelea muuza duka na kumuuliza
Kijana wa kimmasai: Ile soda nyeusi iko? (akimaanisha cokacola)
Muuza duka akifurahia kumpata mteja alijibu
Mpogoro muuza duka: Ndiyo ipo, karibu mteja
Wamasai kwa asili yao ni kama wakenya wengi hawaombi bali wanaagiza, kijana akaagiza soda hivi
Kijana wa kimmasai: Mpe mimi soda.
Kwa aharaka sana mpogoro muuza duka aliileta soda nyeusi na kumuambia
Mpogoro muuza duka: Hii hapa
Kijana wa kimmasai: Fungua
Mpogoro muuza duka: Nimeifungua hii hapa
Kijana wa kimasai akionyesha shilingi kumi alimwambia hivi
Kijana wa kimmasai: Nipimie ya silingi kumi, pesa hii hapa:
Mpogoro akaduwaa, sikujua kilichoendelea baada ya hapo
Vichekesho vya Kesi ya Mmasai na Mpare
Kulikuwa na wizi ulifanyika katika nyumba moja ya mpare pale hedaru na muhusika baada ya kufuatilia aligundua kuwa aliyemuibia ng’ombe wake alikuwa ni mmasai mmoja wa ng’ambo ya pili ya mto kikuletwa.
Mpare alimfungulia kesi ya wizi mmasai na mahojiano mahakamani yalikuwa kama ifuatavyo:
Mmasai; Wewe anasema mimi ameiba hiyo ng’ombe yako?
Mpare; Ndiyo
Mmasai; Aliingia kwa mlango ya nyuma ama ya mbele?
Mpare; Ya nyuma
Mmasai; Mekosa, aliingia kwa mlango ya mbele ya nyumba
Mmasai; Je, aliswaga ng’ombe dume akatangulia mbele au alikuwa nyuma?
Mpare; Dume alitangulia mbele
Mmasai; Mekosa tena, alibaki nyuma
Mmasai; Je ng’ombe alioibiwa iko ngapi?
Mpare; Ng’ombe 7
Mmasai; Amekosa kabisa, ng’ombe alikuwa 5 tu!!
Aha ha ha
Wewe hisi jaji alimhukumu au alimuachia huru huyo mmasai?
Chapati Thief Kansiime Anne – African Comedy
What!!? U have not Subscribed yet??? Eh nga you are a RISK -TAKER!!
NOW NEW CLIPS EVERY TUESDAY AND FRIDAY!!!
pls also like me on facebook
https://www.facebook.com/pages/Kansiime-Anne-Entertainer/263758240421584?ref=ts&fref=ts